Thursday, August 16, 2012

2:18 PM
Timu ya kenya inayo julikana kwa jina la leopard fc-football club itawasili kesho wakiwa tayali kupambana na simba sport club na yanga sport club katika uwanja wa taifa jijini dar-es-salaam mechi ya kirafiki kwa ajilli ya kujianda naligi kuu ya tanzania bara Akizungumzia ujio wa timu hiyo, Mratibu wa mechi
hiyo, Kennedy Mwaisabula alisema kila kitu
kinakwenda vizuri na wanatarajia mechi hizo
zitajaa upinzani mkali kutokana na jinsi timu
hiyo ilivyo.
"FC Leopards ni timu nzuri kila mmoja anaijua
kwani inaupinzani mkali sana katika Ligi Kuu ya
Kenya, na ndio maana tukaiomba ije kwa ajili ya
kuzinoa timu zetu," alisema Mwaisabula.
Kwa upande wake Kocha Mkuu wa Simba Milovan
Cirkovic alisema mechi hiyo itakuwa kipimo kizuri
kwa wachezaji wake wapya kwani ataweza kubaini
mapungufu katika kikosi chake.
"Ni mechi nzuri ambayo naimani kabisa
itaniwezesha kujua mapungufu katika kikosi
changu, hivyo nawataka wachezaji wangu waitumie
vizuri kwani ninafasi nyingine kwao katika
kutafuta namba katika kikosi cha kwanza," alisema
Milovan.
Alisema wakicheza mechi hiyo atatafuta mechi
nyingine zaidi ili aweze kukipika vizuri kikosi
chake, kwani katika michuano ya Kombe la Kagame
aligundua mapungufu mengi.

0 comment.:

Post a Comment