Monday, March 11, 2013

12:06 PM
KOCHA Mfaransa wa Simba SC, Patrick Liewig anaweza kuondoka wakati wowote bila hata kufukuzwa, baada ya maji kumfika shingoni, imefahamika.
Habari za ndani, ambazo Fzakar. imezipata zimesema kwamba Mfaransa huyo ana miezi miwili hajalipwa mishahara na hapo hapo kwa takriban wiki sasa amepokonywa gari.
Gari alilokuwa anatumia kocha huyo ya GX110 linashikiliwa na uongozi wa hoteli ya Spice, iliyopo Kariakoo, Dar es Salaam ambao unaidai klabu hiyo kiasi cha Sh. Milioni 28.
Spice ndiyo kambi kuu ya Simba SC mwaka jana, lakini baada ya deni kuwa kubwa, wakahamia katika hoteli ya Sapphire Court, iliyopo Kariakoo pia ambako nako walifukuzwa jana baada ya deni kuwa kubwa.

0 comment.:

Post a Comment