Tuesday, April 30, 2013

11:20 AM
MTANZANIA APEWA ITC KUCHEZA MSUMBIJI

Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu kushoto, wanacheza DRC. Idadi ya Watanzania wanaocheza nje yazidi kuongezeka

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Yussuf Kunasa kucheza nchini Msumbiji.
Shirikisho la Soka Msumbiji (FMF) lilituma maombi TFF kumuombea hati hiyo Kunasa anayekwenda kujiunga na timu ya Estrela Vermelha da Beira inayocheza Ligi Kuu nchini humo.
Kunasa ambaye msimu huu hakuwa na timu, amejiunga na timu hiyo akiwa mchezaji wa ridhaa.
Zaidi ya wachezaji 10 kutoka Tanzania hivi sasa wanacheza katika klabu mbalimbali nchini Msumbiji.


0 comment.:

Post a Comment