Wednesday, August 29, 2012

7:05 PM

SIMBA imepata ushindi wa 2-1 dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha katika mechi ya kirafiki kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid leo jioni huku magoli yote matatu yakisababishwa na nyota wapya waliojiunga na klabu hiyo ya Msimbazi katika kipindi hiki cha usajili.

Magoli mawili ya Simba yamefungwa na Mghana Daniel Akuffor na Mrisho Ngassa wakati la wenyeji limesababishwa na beki mpya wa mabingwa hao wa Tanzania Bara, Pascal Ochieng, aliyemchezea madhambi mchezaji wa Oljoro ndani ya 18.

Akuffor aliyejiunga akitokea Stella Abidjan ya Ivory Coast, aliifungia Simba goli la kuongoza katika ya 28 kufuatia pasi ya Ngassa na Ngassa, aliyetua Msimbazi kwa mkopo wa msimu mmoja akitokea Azam FC, alifunga la pili katika dakika ya 76 akimalizia pasi ya nyota mwingine mpya Abdallah Juma, aliyeingia katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Akuffor. 

0 comment.:

Post a Comment