Friday, March 15, 2013

9:15 AM
KOCHA wa Simba, Patrick Liewig ametoa onyo kali kwa nyota wake kwa kusema hakuna mchezaji anayeweza kuwa juu ya timu hiyo.
Kauli hiyo imekuja, baada ya hali ya nidhamu kwa wachezaji wa Simba kuwa mbovu na kuchangia timu hiyo kupata matokeo mabaya kwenye ligi.
Mfaransa huyo alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa tatizo hilo ameona zaidi kwa wachezaji 'mafaza'
Hali ambayo imemlazimu kutumia wachezaji watano hadi sita vijana kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
"Nafikiri kama nidhamu itakuwa mbovu kwenye timu. Kamwe hatuwezi kufikia malengo ambayo tumejiwekea."
"Kwa hiyo ni sahihi kwangu kwenda na wachezaji ambao wananielewa ambacho wanatuma kukifanya uwanjani."
"Hakuna mchezaji anayeweza kuwa juu ya timu." alisema kocha huyo aliyerithi mikoba ya Mserbia Milovan Cirkovic.

0 comment.:

Post a Comment