Sunday, March 17, 2013

3:36 PM
AZAM FC imeanza vyema Raundi ya Pili ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF), baada ya usiku huu kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji Barrack Young Controllers katika mchezo wa kwanza wa hatua hiyo uliofanyika kwenye Uwanja wa Antonette Tubman Monrovia, Liberia.
Kwa matokeo hayo, Azam sasa itahitaji hata sare tu ili kusonga mbele, Raundi ya Tatu na ya mwisho ya mchujo kabla ya hatua ya makundi.
Shujaa wa Azam FC leo alikuwa ni Seif Abdallah Karihe aliyefunga bao la ushindi dakika ya 90, kufuatia kazi nzuri ya Khamis Mcha ‘Vialli’.
Katika mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Farouk Mohamed kutoka Misri, hadi mapumzikko, B.Y.C. walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililofungwa na
Azam wangeweza kuondoka uwanjani baada ya dakika 45 za kipindi cha kwanza wakiwa wana mabao, kama wangeweza kutumia nafasi nzuri takriban sita walizopata.

0 comment.:

Post a Comment