Monday, August 20, 2012

6:59 PM
Mbwana Ally Samatta anazidi kung'ara kwenye soka la anga ya kimataifa akiwa na klabu yake ya TP Mazembe.

Mbwana Samatta ambaye tayari anatimiza mwaka mmoja tangu ajiunge na timu yake hiyo ya Kinshasa Congo akitokea klabu bingwa ya Tanzania bara Simba Sports Club, amekuwa mmoja ya wafungaji bora na tegemeo kabisa kwenye timu hiyo inayomilikiwa na tajiri Moise Katumbi.

Kwa takwimu zilizo sahihi kabisa za Mbwana Samatta katika msimu huu 2011/12 upande wa Ligi ya mabingwa wa Afrika amecheza mechi 7 tu.

Katika mechi hizo saba Samatta "Golden Boy" amefunga mabao 5. Katika magoli hayo matano, kichwa chake kimeweka kambani mabao 4 na moja amefunga kwa guu lake la kulia.

Mabao hayo matano ya Samatta kwenye Africa Champions league amezifunga timu za Power Dynamo akiwa Ugenini, Akafunga bao lingine dhidi ya Al Merreikh aTP wakiwa nyumbani kabla ya kuja kuwafunga tena Wasudan hao nyumbani kwao Khartoum. Alhly wakawa majeruhi wengine wa Mbwana Samatta baada ya kuwaumiza wakiwa kwao Misri. TP Mazembe wakiwa uwanja wao nyumbani Tanzania Golden Boy akatupia bao moja kwenye mechi dhidi ya Berekum Chelsea. Ikafika zamu ya waarabu Zamalek ambaye akawafunga bao moja moja nyumbani na Ugenini na kutimiza mabao matano.

Dakika ambazo Mbwana Samatta anafunga sana magoli ni kuanzia kati ya dakika ya 16-30 ambapo hapo amefunga mabao mawili. kuanzia dk ya 31 mpaka 42 amafunga goli moja tu, huku akionekana kuwa hatari zaidi kwenye dakika ya 75 ya mchezo kwani tayari ameshafunga mabao mawili kwenye dakika hiyo.


Mafanikio hayo ya Samatta kwenye michuano mbalimbali TP Mazembe inayoshiriki yamezidi kumuongezea thamani kwenye soko la usajili duniani, kutoka kuuzwa kwa dola 100,000 na Simba kwenda TP Mazembe mpaka sasa anakadiriwa kuwa na thamani ya £175,000 ambayo ni mara 3 ya zaidi TP waliilipa Simba kumsaini Samatta.

0 comment.:

Post a Comment